0
Alan PardewHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionAlan Pardew
Kiungo wa kati wa Real Madrid na mjerumani Toni Kroos, 28, ni lengo kuu la Manchester United, ikitaka achukue mahala pake Michael Carrick ambaye anastaafu msimu ujao. (Independent)
Alan Pardew anajaribu kuokoa kazi yake huko West Brom na kipigo walichokipata kutoka Huddersfield siku ya Jumapili kinaweza kumaliza kuwepo kwake katika klabu hiyo baada ya wiki 12 tu.
Wilfried ZahaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWilfried Zaha
Tottenham ina mpango wa kufanya jitihada mpya kumpata wing'a wa Crystal Palace Wilfried Zaha, 25. Klabu hiyo ya Mauricio Pochettino ilishindwa baada ya kujaribu mara mbili kumpata mchezaji huyo raia wa Ivory Coast. (Mirror)
Paris St-Germain hawana nia ya kumsaini mlinzi wa Manchester United Marcos Rojo, 27, licha ya kuhushwa na mpango wa pauni milioni 30 na mchezaji huyo wa Argentina. (ESPN)
Marco AsensioHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMarco Asensio
Kiungo wa kati wa Real Madrid Marco Asensio, 22, anasema amepata ofa kutoka vilabu vitano vikiwemo Liverpool, Chelsea, Arsenal, Bayern Munich na Juventus, lakini rais wa klabu ya Florentino Perez hataki kumuuza raia huyo wa Uhispania. (Diario Gol - in Spanish)
Ajenti wa Nabil Fekir amekataa kuthibitisha ikiwa kiunga huyo wa kati wa Ufaransa ambaye amelengwa na Arsenal atajiunga na Lyon msimu ujao. (Telefoot via Mirror)
Leonardo UlloaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionLeonardo Ulloa
Mshambuliaji wa Argentina Leonardo Ulloa, 31, anasema anataka kufanya kuhama kwake kwa mkopo kutoka Leicester kwenda Brighton kuwa wa kudumu mwisho wa msimu. (Argus)
Klabua ya Sunderland imetangazwa kuzwa kwa pauni milioni 50. Klabu hiyo imekuwa ikizushwa ngazi mara kwa mara. (Mirror)
Kylian Mbappe atakamilisha kuhama kwake kwa pauni milioni 166 kutoka Monaco ikimaanisha kuwa PSG watamnunua mchezaji huyo wa miaka 19 raia wa Ufaransa baada ya kuepuka kuzushwa. (Mail)
Eliaquim MangalaHaki miliki ya pichaREX FEATURES
Image captionEliaquim Mangala
Everton itabaki bila ya mlinzi wa kukopwaa wa Manchester City Eliaquim Mangala kwa msimu wote baada ya mlinzi huyo mfaransa kupata jeraha wakati wa ushindi dhidi ya Crystal Palace. (ESPN)
Meneja wa West Bromwich Albion Alan Pardew ana mechi mbili za kuokoa kazi. (Sun)
Paris St-Germain wanafikiria kutumia pauna millioni 30 kumsaini mlinzi wa Manchester United Marcos Rojo, 27. Mkataba wa raia huyo wa Argentina huko Old Trafford unafikia mwisho msimu ujao. (Sun)

Post a Comment

 
Top